Kenya 🇰🇪 Teachers Are The Most Well Paid In East Africa

Image
ANALYSIS By Dorris Otieno Kenyan teachers are not only the best paid in East Africa, but also earn almost 12 times more than the country's average pay, a comparative study by Nation Newsplex and the Institute of Economic Affairs reveals. Even as teachers go on strike for the 12th time since their first industrial action in 1962, the analysis, which compares teachers' salaries in Kenya with those of their peers in select African countries , also finds that the lowest-paid teacher in Kenya earns more than the highest-paid teacher in Uganda. Uganda and South Africa were chosen as countries against which to compare wages of teachers because they have the most up-to-date data against which the comparison could be made. While Tanzania was not included in the comparison because only average pay for the year 2011 was available, even its figures indicated that Kenyan teachers earn more than their Tanzanian counterparts. The highest paid Kenyan teacher earns almost 12 times more than the

NJIA 8 ZA KUONGEZA MAHUSIANO MAZURI FACEBOOK NA KUIMARISHA BIASHARA YAKO






Kulingana na Utafiti uliofanywa na "Creative Group", 50% ya Maafisa Masoko kwenye Makampuni walisema wanategemea kuongeza uwekezaji Facebook mwaka huu.

Facebook ni rahisi, unaboresha ukurasa wako wafuasi watafurika haraka sana na kujibu! Hiyo ni ndoto ya kila mwenye kuingia hapa kabla hajaanza au ndivyo alivyosikia kutoka kwa watu wanaodai ni Wataalamu katika fani hii. Wengi  wao uishia Kutelekeza Kurasa au kuacha wasipoona matokea mazuri wanayotarajia licha ya kutuma taarifa mara kwa mara! Hapa nikupe ukweli; watu hawahitaji kusikia au kuona bidhaa yako mara kwa mara. Kwa nini wasikie au waone wakati muda wote wanakuwa wamerundikiwa na Matangazo kutoka Mbaoni, TV, Radio ata mtu anapotembelea mtandao wa Inteneti. Ngoja tukabiliane na ukweli huu; watu hawaji  Facebook kuona matangazo. Kinachowaogopesha wenye kutangaza ni kuwa Facebook imetengenezwa ikimpa mtumiaji nguvu ya kutawala, hivyo anaweza kuamua kulidharau na kuliacha kando Tangazo lako akiamua kufanya hivyo. Kuongeza mahusiano mazuri Facebook unahitajika kuandika vitu vyenye maudhui matamu na vya kipekee. 

Kulingana na Uzoefu nilionao na kutumia wengine walionitangulia katika fani hii, nitakupa njia zilizonisaidia kuongeza mahusiano kwenye Ukurasa wangu na nilichoona kimewasaidia wenzangu.

1. Uliza Maswali
 
Maswali ni njia muhimu ya kuchochea mazungumzo na washabiki wako. Uenda ndio njia rahisi ya kuwafanya watu wajihusishe na unachokituma. Kuna maswali mengi ya kuweza kuwauliza washabiki wako,

2. Muda wa Kutuma 

Muda wa kutuma "posts" ni muhimu sana kwenye Mitandao ya Kijamii. Fikiria unatuma ujumbe muda ambao kila mtu yupo kazini au yupo usingizini . Ni vema kutuma ujumbe wakati watu wamemaliza kazi au wapo kwenye usafiri wanarudi nyumbani. Hizi ndizo nyakati watu utembelea akaunti zao kwenye mitandao ya kijamii kuona kinachotumwa na wenzao. Kulingana na Dan Zarella, muda mzuri wa kutuma post kwenye Facebook ni mchana na muda kidogo kuanzia SAA 1 Jioni.

3. Picha

Tunaambiwa kuwa Picha uwakilisha maneno elfu, kweli? Kwenye Facebook Picha ina maana zaidi ya maneno elfu moja. Picha lazima zitumiwe kurahisisha mawasiliano na mahusiano kwani usimamia vizuri kuliko Jumbe nyingine au links. Picha uwa wazi na fupi na rahisi kueleweka. Leneys, kampuni ya mitindo kwa akina mama utuma Picha nyingi na kuwaomba washabiki kuchagua mitindo wapendayo. Matokeo yake ni makubwa. Post hii tu iliwapa 51 komenti, 52 likes na 55 shares kutoka kwa fans na wakiwaomba marafiki wao wasambaze na kushirikisha wengine!

4. Mashindano ya Facebook

Mashindano ni njia muhimu ya kuongeza mahusiano kwenye mtandao wa kijamii wa Facebook
kwa sababu siyo tu inawazawadia wafuasi watiifu lakini inaleta hamasa kwa watumiaji kutembelea Ukurasa wako mara kwa mara ili kuona kama wameshinda. Kuna mashindano ya aina nyingi unaweza kuendesha. Matangazo katika Mitandao ya Kijamii, mfano, Binkd, siyo tu yanaruhusu kujenga shindano la ukweli na uwazi, lakini yanaleta changamoto kwenye kujenga mahusiano. Mashindano tofauti yanaweza kukusaidia kulenga mahusiano utakayohitaji kutoka kwa hadhira na watu unaowahitaji. Mashindano ya 'Kura ili Ushinde' yatakuletea 'likes' nyingi, lakini siyo komenti nyingi kama mashindano mengi yenye kuleta changamoto kubwa yatakufanya uandike tagline kwenye kisanduku cha kutoa maoni. Mari Smith siku za karibuni aliendesha Shindano lililofanikiwa kwa kutumia Strutta.  Shindano lake lilipata ingizo zaidi ya 392 kutoka kwenye washiriki maalum 377.  Shindano lake pia liliingiza kura 15,571 kutoka kwenye wapiga kura maalum  2,153.  Moja ya Ujumbe wake alioutuma kwenye shindano ulipata zaidi ya ushirikishaji 50, maoni  42 na liki 150 na hiyo ni positi moja tu!

5. Majibu kwa Kutumia "Crowdsource"

Kuliko ujibu maswali mwenyewe , kwa nini husitumie Marafiki wako wawasaidie wengine wanaohitaji maelekezo  na ushauri? Hivyo ndivyo Natural Parenting Tips, Ukurasa wa Facebook ambao umejitoa kuwasaidia Wazazi/Walezi unafanya.  Kila siku bila kuacha uuisha ukurasa na maswali kutoka kwa marafiki. Wazo hapa ni kutumia Crowdsource kwa vidokezo kutoka kwa Wafuasi wako,ambao husaidia kushauri wengine.

6.Wito kwa Vitendo

Wito kwa Vitendo unawawezesha wanamasoko mtandao kisaikolojia kuwatumia Wafuasi wao kwa namna wanavyotaka. Kitu tunachokosea mara kwa mara ni kusahau kuuisha WITO KWA VITENDO ( CALL TO ACTION) kwenye Kurasa zetu za Facebook. Hadhara yako uwa inaitikia vizuri kama imeelekezwa namna ya kuitikia.Unataka watu wafanye nini? Watoe maoni gani? Wabonyeza kifungo? Washiriki jambo na wenzao? Subway, kampuni ya kimarekani inajua vizuri maana ya WITO WA VITENDO! Kila mara kwenye ukurasa utakuta wanawaelekeza wateja kitu cha kufanya, Mfano like hapa, washirikishe wenzako, Bonyeza, hii pekee iliwasaidia kupata Likes 53,000 na shares 404.

7..Matangazo ya  Facebook 

Ukiona namba ndogo ya watu ndiyo inatembelea Ukurasa wako,nini utafanya kuongeza namba  inayotembelea ni kuanza na Tangazo la Facebook. Hii inasadia kuwafikia watu wengi kwa muda mfupi

8. Mpangilio wa Kutuma Ujumbe ( Frequency Of Posting)

Mpangilio wa kutuma positi zako nao una maana kwenye Mahusiano na Washiriki wako Facebook. Tukirejea kwenye Utafiti wa Buddy Media, Kurasa ambazo uwa zinatuma Ujumbe mara mbili kwa siku upata 40% ya mahusiano ya juu kuliko wale wanaotuma mara 3 au zaidi kwa siku. Hii inaonyesha kuwa kinachomata siyo Idadi bali Ubora wa kinachotumwa Facebook. Jambo moja linaweza leta mafanikio kwa mtu mmoja na si lazima liwe hivyo kwa kila mtu.Unahimizwa kujaribu njia hizi ili uone ni ipi inafanya kazi kuliko nyingine







Comments

Popular posts from this blog

LinkedIn: A Social Networking Site for Business People and Professionals To Connect

The Tanzania Government Invites You To Discover Some Compelling Reasons To Invest.

Investment Opportunities in Integrated Waste Management in Tanzania